Thursday 10 September 2015

Waislam Tujihadhari na Kundi ili.

Miaka hii ya karibuni kumejitokeza baadhi ya watu, wakijitambulisha kwa mabandiko na picha mbalimbali za wapiganaji walioko uko Syria na Iraq, kwa jina maarufu ISIS.

Kwa mtazamo wa juu kwa juu, unaweza kuona kuwa watu hao wanapigania kuwepo na serikali ya Kiislam kwa maana ya khilafa na kabla ya hapo walijitangazia kuwepo kwa Majimbo ya Kiislam yaani Islamic State.

Kuna baadhi ya wanao jiita waislam kwa makusudi kabisa na kwa malengo yao maalumu wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii kuwashawishi watu wawaunge mkono watu hawa. Na matokeo yake vijana wengi wameishia kukamatwa na vyombo vya usalama na kuozea jela.

Turudi nyuma kidogo na tutazame hawa wanao jiita Islamic state, wameanzaje na imekuwaje mpaka wamepata umaarufu kwa kipindi cha muda mfupi?
Mambo yote haya yemeanzia uko Iraq, baada ya serikali ya Sadam Hussein kuondolewa madarakani na kukaachwa kitu kinachoitwa Power vacuum (https://en.wikipedia.org/wiki/Power_vacuum), kwa maana ya kutokuwa na uongozi au waliokuwepo madarakani wanakuwa hawana uwezo wa kuongoza kiasi ya kujitokeza makundi makundi ambayo ujichukulia sheria na madara na kuongoza kwa namna wanavyo taka wao.

ISIS wameanza harakati zao mwaka 2006 katika moja ya vikundi vidogo vidogo ambavyo vilianzishwa kusaidia kusaka mabaki ya askari wa Sadam Hussein nchini Iraq. Kikiwa kikundi kidogo tu, kisicho kuwa na siraha za hatari kama walizonazo hivi sasa.

Ifahamike kwamba siku zote serikali ya Marekani, utafuta visingizio vya kushambulia nchi wanayotaka kuiba rasilimali zake au inapo ona kuwa kuna hatari ya kupoteza vyanzo vyake vya kiuchumi, na hapa kinacho zungumziwa ni Mafuta.

Nchi ya Marekani kuishambulia Syria moja kwa moja lingekuwa swala gumu na gharama zake zingekuwa na ukizingatia gharama walizo zitumia kwenye vita ya Iraq zilikuwa bado kurejeshwa. Na hapo hapo ndani ya Marekani hali ya kisiasa haikuwa nzuri kwa upande wa serikali iliyoko madarakani.
Ndipo wakaona kuyatumia makundi yalioko Syria, ili wawasaidia kuiondoa serikali iliyoko madarakani. Makundi haya yalionekana kuwa na misimamo tofauti na ile ambayo nchi za Kimagharibi zinataka, haya makundi yalitaka kuanzisha serikali ya Kislamu nchini Syria tu tofauti na ISIS, wao wakaja kuteka wazo na harakati zima zilizokuwepo na kujitangazia wao kuwa ndio wenye jukumu ilo.

Ndipo mwaka 2009 ISIS wakaitwa kwenda Syria ili kusaidia kumuondoa madarakani rais wa Syria Bashar Hafez al-Assad. Na lengo haswa halikuwa kumuondoa bali kuharibu harakati ambazo tayari zilikuwa zimeanzishwa vikundi vingine ambavyo vilisha anza kujipatia umaarufu kama vile Jabhat al-Nusra (al-Nusra Front) na Al-Jaysh (Free Syrian Army). Na hata ikitokea kundi au nchi yoyote ile kutangaza Khirafa basi ionekane kuwa utawala huo utakuwa ni wa kiuonevu na umwagaji wa damu. Kama vile tunavyo ona ISIS wakiwafanyia raiya wasi na hatia.

ISIS ndipo walipoanza kupata pesa na mafunzo rasmi ya mbinu za medani na ujanja wa kupigana mitaani kutoka kwa majeshi ya Amerika na washiriki wake kama Israel, Saudi, Jordan, Qatar, Uturuki, na Uingereza.

Rais Obama alipo hojiwa kuhusiana na kuviunga mkono vikundi vinavyoipinga serikali ya Bashar, alisema kuwa wanachowasaidia ni ushauri wa kiufundi na kutoa misaada ya kibinadamu tu. Kumbe kinyume chake walikuwa wakiwapatia pesa na siraha ambazo Marekani waliziacha Iraq, kama vile magari ya deraya, vifaru, mizinga ya kutungulia ndege na siraha nyingine nyingi.

Senate John McCain, alipo hojiwa alisema vita vya kuwapiga magaidi zinatarajiwa kudumu kwa miongo kadhaa, yaani si chini ya miaka thelathini.
Mwezi wa September 2013 habari zikaandikwa kwenye vyombo vya Kimarekani kuwa siraha ambazo USA kwa kutumia shirika lake la Kijasusi (CIA) wameweza kuwafikishia siraha na misaada mingine makundi yanayoipinga serikali ya Bashar, wakati huo huo kundi la Al-Jaysh (Free Syrian Army - FSA). Wakapinga kupata msaa wa siraha zozote kutoka serikali ya Marekani, japokuwa walikuwa wameahidiwa kupatiwa siraha. 



Wachunguzi wa habari za kimataifa wakajiuliza, siraha zimekwenda wapi, mbona makundi yaliokusudiwa yanalalamika kuwa hawakupata siraha. Serikali ya Marekani ikasisiza kuwa siraha zimekwisha wafikia walengwa. 

Haikuchukuwa muda mrefu ndipo mwezi Juni 2014 ISIS walipojitokeza wakiwa na siraha nzito uku wakiwa wamehitimu mafunzo ya kivita kutoka serikali ya Marekani na Israel. Na hata zilipotoka picha ambazo ISIS walipiga wakionyesha kuwa wameteka vifaru na siraha nyingine mbalimbali, nchi za Kimagharibi na haswa Marekani hawakuonyesha kushtuka, kwa sababu ilikuwa ni zawadi kutoka kwao.

ISIS ndio kundi tajiri la kipekee duniani, taarifa za kiuchunguzi zinasema kuwa licha ya misaada ya kifedha kutoka nchi zinazowaunga mkono, pia wanauza mafuta kwa kiwango kikubwa pato lake linakisiwa kwa siku kuwa ni zaidi ya dola za kimarekani milioni 1 kwa siku na fedha zingine zifikiazo dola milioni 20 zipatikano kwenye utekaji nyara na mapato mengine.


Marekani kwakutaka kujisafisha ikapiga baadhi ya visima vya mafuta na kuacha makampuni yenye kununua mafuta kutoka kwa ISIS yakiendelea kufanya biashara nao.

Wakati huo huo upande mwingine serikali ya Marekani inataka vita vya Syria viendelee muda mrefu, kwa sababu wanafaidia kwa upande mwingine, wanacho kifanya ni kuwapa pesa wapiganaji wa FSA ili vita iweze kuendelea muda mrefu, inakisiwa pesa walizopata ni dola za Kimarekani zipatazo milioni mia tano. Kundi ili alipewi siraha kama walizopewa ISIS kwa sababu watakapopewa siraha kuna uwezekano mkubwa wa ISIS kushindwa vita, kitu ambacho Marekani haitaki kitokee.


Waungaji Mkono

Wakati huohuo ili kundi liweze kupata kuungwa mkono na Waislam wasio jitambua au kuelewa kinacho endelea. Wameweza kulinasibisha kundi ili na Uislam na kuwa wanapigana Jihad kwa manufaa ya Uislam duniani. Hapo hapo wamesahau kuwa ISIS (Islamic State of Iraq and Syria) au ISIL (Islamic State of Iraq and the Levant) Neno Levant hapa linakusanya nchi Lebanon, Syria, na Israel. Wenyewe wanapigana kwa malengo mengine na uku wakijitambulisha kutaka kuzikomboa nchi zilizoko kwenye majina yao ambazo ni Iraq, Lebanon, Syria, na Israel.

Lakini ajabu utawakuta vijana wachache wasio jitambua, wanashinda kwenye mitandao ya kijamii, wakiwaunga mkono ISIS.

Haiwezekani kwa Muislam awe anauwa Waislam wenzake kisha ajitambe kuwa yeye ni Muislam, kisha watokee watu wawaunge mkono uku wakiwa na vijisimu vyao vya mkononi na wakijifanya kuwataka watu wakapigane upande wa Isis na Al-shabab.

Waislam wachache awa ambao wanatumiliwa na nchi za Kimagharibi ili kuonyesha kuwa wanapiga vita Ugaidi, lengo ni kuwaridhisha wananchi wao ambao ndio walipa kodi kuwa wanapiga vita ugaidi sin je ya nchi tu, hata ndani ya nchi zao.

Ndio ikaundwa program maalum ya kuwafundisha baadhi ya mashushu, ili kutafuta nani na nani wanaelekea kuwaunga mkono ISIS na magaidi wengine. Ndipo wakatengenezwa Waislam wasio jitambua au wenye kuendekeza matumbo yao, wakakesha mitandaoni na kujifanya kuwa wana uchungu sana na Uislam na wanawaunga mkono ISIS, ili hali wao wenyewe hata uwanja wa vita hawaujui unafananaje.

Mashushu awa uwa hawakamatwi, hata wakijitokeza hadharani na kuonyesha wazi kuunga mkono harakati za ISIS, Wanao kamatwa ni wale walioingia mkenge na kudhani kuwa wanakwenda kwenye JIhadi ya kweli kumbe ni kanyaboya. Wakisha wapata watu ambao wanaona kuwa wanawaunga mkono Alshabab au ISIS haraka sana wanawaripoti kwa mabwana zao na mara uishia jela.

Na hii ndio mbinu zinazotumika hivi sasa za kujifanya wanapambana na siasa kali (extremist) lakini kwa kuwa hakuna Uislam wa namna hiyo ndio kukawa na watu maalum kama hao ambao kazi yao ni kuangalia nani na nani wanaweza kuwashawishi. Wakisha wapata uweza hata kuwapa mafunzo na mbinu hafifu za hapa na pale, kisha kuwapatia tiketi za kugushi na kuwaelekeza waende viwanja vya ndege ili waende Syria. Lakini ghafla vijana hao ujikuta wapo mikononi mwa vyombo vya uslama na habari zao kuandikwa kwenye vyombo vya habari kuwa ni magaidi walikuwa wanakwenda Syria kusaidia ISIS au Alshab. Na raiya wan chi za ulaya wakiona hivyo uona kuwa serikali zao zinafanya kazi vyema za kuwalinda na magaidi wan je ya nchi na hata wa ndani ya nchi.

Hii inafanyika sana kwenye nchi za Uisngereza, Ufaransa na Marekani na nchi zile zinazopiga vita Uislam kivitendo.

Ukikutana nao vibaraka hawa wa kimagharibi, utasikia wakisema ISIS wanauwa Makafiri, Wanafiki na Washirikina, sasa tunawauliza. Kama mtume angeua Makafiri na washirikina wote wa Makkah sijui nani angebakia. Waislam waliokuja Afrika nao wangeua Makafiri na Washirikina wote walio wakuta, sijui mimi na wewe kama leo tungekua hapa, ni jambo lililo wazi kabisa babu wa babu zetu wangekuwa maiti na hata mimi na wewe tusingepata hata hii nafasi ya kuwa Waislam, maana ukiangalia wengi tunaweza kukuta Mababu zetu walisilimu kwa kuona tabia njema za hao walikuja na Uislam na ndio wakaupenda na kusilimu.

Kama utakuwa mfuatiliaji mzuri wa makundi haya, utaweza kugundua kuwa makundi yote haya ni zao la Mmarekani na lengo ni kudhoofisha nchi zenye Waislam wengi ili wapate kuchukua wanacho kitaka kiurahisi.

Ndio tukaona uko Iraq walipoweza kuangusha serikali jambo la kwanza kufanya ni kulinda kwa nguvu zote vyanzo vyote vya mafuta. Na wkafanya hivyo hivyo nchini Libya.

Sasa wanasubiri Syria iangue rasmi kisha utaona wanapeleka majeshi kujifanya kuweka mambo sawa kumbe wanafata wanao yafata.


0 comments:

Post a Comment

Je Una Nasaha zozote Kuhusiana na Makala hii?

RAMADHAN KARIM

Read

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!