Friday 30 June 2017

JE NA WEWE UNASUMBULIWA NA TATIZO LA UTEJA?

Uteja wa Simu Hauna Tofauti na Utumiaji wa Madaya ya Kulevya

Unaweza kukataa kuwa wewe si TEJA, kwa sababu tu, umewahi kuwaona watu walio athirika na matumizi ya madawa ya kulevya haswa vijana, jinsi walivyo dhohofika.

Ukiwaangalia MATEJA WA MADAWA YA KULEVYA, wanapoyakosa kutumia madawa, mihili yao uingia kwenye taharuki na hofu inayoambatana na mbabaiko wa moyo kupaparika.

Wanakuwa ni wenye hasira na wakati mwingine wapo tayari hata kukwapua mali za watu ili wakanunue madawa hili watulizane na nafsi zao.

Lakini hata wewe na mimi, wakubwa kwa wadogo, wazee kwa vijana tunaweza kujikuta tupo kwenye kundi la UTEJA ambao si rasmi, lakini limekuwa ni tatizo lililo wakumba watu wengi.

Waweza kukataa kuwa wewe si TEJA, sawa tunaweza kukubalia...

MASWALI YA KUJIULIZA:
1. Je Ulishawahi kupoteza SIMU yako au Kuhisahau Mahali?
Je, ile hali nawe haikukupata ya taharuki na hofu inayo ambatana na mbabaiko wa nafsi/moyo kupaparika na kukosa raha kuliko pitiliza?

2. CHA MWANZO NA CHA MWISHO
Je, simu zetu atupandi nazo vitandani na kuwa ndio ktu cha mwisho kukitumia kabla usingizi haujatupitia?

4. MESEJI ZA SAA TISA USIKU
Je, ni mara ngapi umeamka saa nane au tisa za usiku na kitu cha kwanza ni kufungua simu yako kuanza kutuma meseji kwenye magroup!?

5. SIMU UMEIGANDA
Je, ni mara ngapi umejikuta unaingia msalani, kisha ukakumbuka kuwa simu umeiwacha mezani ukairejea na kuingia nayo chooni.

6. WASIWASI WA KUTOPTWA
Je, ni mara ngapi katika nusu saa umeifungua simu yako hata kama hakuna meseji iliyoingia?
Je, ukuwahi kupata wasiwasi labda simu mbovu kwa kuwa tu, saa nzima imepita bila meseji kuingia kwenye simu yako?
Ni mara ngapi umesisitiza kwenye group kuwa group limepooza kwa kuwa tu hakuna meseji mpya?

7. SIMU KABLA YA SWALA
Ni mara ngapi umekuwa kwenye nyumba ya IBADA na kabla ya kuanza Kuswali, ukajikuta unaangalia kwanza simu kama kuna meseji?
Ni mara ngapi umehisi mtetemeko wa simu mfukoni na uapoiangalia ukuti meseji, kumbe ni wasiwasi wako tu!
Na ni mara ngapi umefungua simu yako mara tu baada ya kumaliza swala yaani kitu cha kwanza tu umalizapo kuswali kikawa ni simu?

8. KUTOJIWEZA BILA SIMU
Swali la kujiuliza hapa, Je! Waweza kukaa saa ishirini na nne (24) bila ya kuwa na simu yako?

9. FIKIRIA KWA MAKINI
Mara ngapi umepata habari hata ujaithibitisha, unairembea kwenye group na kuanza kuitetea kuwa ni ya kweli na ilihali ndani ya nafsi yako unajuwa kabisa kuwa hiyo habari ujaithibitisha na wala huji chanzo chake!

Kama hayo au baadhi ya hayo yalio andikwa hapo juu yamekukuta, basi ujuwe na wewe ni TEJA!

Kwa sababu SIMU nazo ni KASUMBA ya KIDIGITARI (Electronic Cocaine/Digital Heroin), kama zilivyo kasumba na uteja wa kutumia madawa ya kulevya.

0 comments:

Post a Comment

Je Una Nasaha zozote Kuhusiana na Makala hii?

RAMADHAN KARIM

Read

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!