Sunday 24 April 2022

MOYO WA MWANADAMU
NDANI YA QURAN TUKUFU

Moyo Wako Una Akili na Hautegemei Ubongo Kufikiri.

Imeaminika kwa karne nyingi kwamba moyo ni sawa na pampu tu inayosukuma damu chafu kwenye mapafu ili ikasafishwe, Kisha inapokea damu iliyosafishwa na kusukumwa sehemu mbalimbali za mwili wa binadamu.

Hivi Karibuni Madaktari wa upasuaji wa moyo na wale wa magonjwa ya akili wameanza kuhakiki imani hiyo. Mwanzoni mwa karne ya ishirini na moja, idadi ya madaktari hawa waliwenza kutambua kwamba wagonjwa wanaopandikizwa moyo hupata mabadiliko kadhaa ya kisaikolojia, kihisia na kitabia. Ambayo hawakuwa nayo kabla ya operesheni.

Hii ilizua shauku yao ya kufuatilia suala hili, na wakaja kugundua ukweli kwamba, Moyo una nishati maalum ambayo husaidia huhifadhi habari na taarifa mbalimbali anazopitia binadamu.

Moyo hubeba hisia na tabia za mmiliki wake wa awali. Kwa hiyo, mara tu mchakato wa uhamisho ukikamilika, Moyo uachia hisia na kumbukumbu kama mkondo wa habari iliyohifadhiwa ndani yake, huanza kutiririka kutoka kwenye moyo hadi kwenye shina la ubongo wa mtu anayehamishiwa Moyo wa mtu mwingine. Hapo ndipo mtu upata hisia ambazo hazikuwepo kabla.

Kwa hiyo, Qur’ani Tukufu, miaka elfu moja na mia nne iliyopita, iliashiria katika nyingi ya aya zake kwamba moyo una idadi ya kazi muhimu katika mwili zaidi ya kusukuma damu.

Moyo ndio mahali pa imani au upingaji, mahali pa busara na hekima, mahali pa papara na uzembe, mahali pa utambuzi au ufahamu, na mahali pa Usalama au uovu, na mahali pa nia njema na nia ovu ndio sehemu ya mgongano juu ya imani ya chaguo zuri au baya, au Kujikurubisha kwa MwenyeziMungu kwa toba au kuhasi, mahali pa kulipiza kisasi, mahali pa kumbukumbu na uchaguzi wa maneno.

Moyo ndio kughafilika, ndio mahala pa mapenzi, rehema na huruma, au chuki, dhulma na ukatili, na pahala pa uongofu au upotofu, na pahali pengine pasipo hapo.

Masuala ya kihisia ya kushikamana yanaunda tabia ya mwanadamu. Amali za waja ni ima kuzitakasa na kiungo cha kukitakasa ni Nyoyo zetu.

Qur'ani Tukufu ambayo iliteremshwa zaidi ya karne 14 zilizopita inasisitiza kwamba Moyo wa mwanadamu ni kiungo chenye hisia na chenye uwezo wa kuhisi, kufikiri na kufanya maamuzi. Sifa kama hizo za Moyo zimegunduliwa hivi majuzi tu katika karne ya ishirini na mwanzoni mwa karne ya ishirini na moja.

Lakini hayo yote yalishatajwa Kwenye kitabu kilichoteremshwa katika karne ya saba, kwa Mtume asiyejua kusoma na kuandika, katika jamii isiyo na elimu kueleza ukweli huu kwa lugha sahihi kabisa ni ushuhuda hai kwa asili ya Kiungu ya kitabu hicho na Utume sahihi wa mpokezi wake.

Kwa mujibu wa Quran, Moyo ni chombo cha utambuzi. Kimsingi mlengwa wa jumbe kuu za Qur'an ni Moyo wa Mwanadamu. Ujumbe unaosikika tu kutoka Moyoni na hakuna masikio mengine yanayoweza kuusikia.

Kwa hiyo Qur'an ina msisitizo mkubwa juu ya kuhifadhi na kuendeleza kiungo hiki. Qur'an mara kwa mara inazungumza kuhusu masuala kama vile utakaso wa Moyo, nuru ya Moyo na werevu wa Moyo.

Ndani ya Qur'ani Tukufu, Moyo wa mwanadamu umetajwa si chini ya mara 132, MwnyeziMungu anasema kwenye Qur'an:

Surat Al-Muuminun (23): 60

Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali Nyoyo zao zinagopa kwa kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi.

Surat Al-Muuminun (23): 78

Na Yeye ndiye aliye kuumbieni kusikia na kuona na Nyoyo za kufahamu. Ni kuchache mno kushukuru kwenu.

Qur'an Suurat Ar-raa'd (93): 28

Wale walio amini na zikatua Nyoyo zao kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Hakika kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu ndio Nyoyo hutua! 

Suurat Al-A'raaf (7): 100

Je, hawahidiki hawa wanao rithi ardhi baada ya wale wenyewe kwamba tukitaka tutawapatiliza kwa madhambi yao, na tutapiga muhuri juu ya Nyoyo zao, na kwa hivyo hawatasikia?

Suurat Al-A'raaf (7): 101

Miji hiyo, tunakusimulia baadhi ya khabari zake. Na hapana shaka Mitume wao waliwafikia kwa hoja zilizo waziwazi. Lakini hawakuwa wenye kuamini waliyo yakanusha zamani. Namna hivi Mwenyezi Mungu anazipiga muhuri Nyoyo za makafiri.

Suurat An'aam (9): 110

Nasi twazigeuza Nyoyo zao na macho yao. Kama walivyo kuwa hawakuamini mara ya kwanza, tunawaacha katika maasi yao wakitangatanga.

Suurat Al 'Imran (3): 151

Tutazitia khofu nyoyo za walio kufuru kwa vile walivyo mshirikisha Mwenyezi Mungu na washirika ambao hakuwateremshia hoja yoyote. Na makaazi yao ni Motoni; na maovu yaliyoje maskani ya wenye kudhulumu!

KAZIYA MOYO SI KUSUKUMA DAMU TU.

Utafiti wa Kisayansi kuhusu Moyo uliofanyika hivi karibuni umethibitisha kwamba Moyo wa mwanadamu huhifadhi na kuchakata taarifa, kama ilivyoripotiwa katika uvumbuzi mpya wa kisayansi na katika Qur'ani Tukufu na maelezo ya hapo juu.

Wataalam wa Moyo wanakielezea kiungo hiki kuwa kina uwezo mkubwa wa kufikiri na ni kitovu cha hisia na mihemko, fikra na mantiki, pamoja na dira na kufanya maamuzi yake bila ya kutegemea Ubongo.

Moyo wa mwanadamu una hisia zaidi kuliko Ubongo wa mwanadamu, ambao unawasiliana nao kwa njia kadhaa na kuathiri uwezo wa kufikiri wa Ubongo, Moyo una uwezo wake wa kukubali, kukataa, kuelewa na kuhifadhi ujuzi.

Moyo hauhitaji Ubongo, au mwili hili ufanye kazi au kuendelea kupiga. Moyo una mfumo wake wa umeme unaosababisha kupiga na kusukuma damu. Kwa sababu ya hili, Moyo unaweza kuendelea kupiga kwa muda mfupi baada ya mtu kufa, au baada ya kuondolewa ndani ya mwili. Moyo utaendelea kupiga maadam kuna oksijeni.

Si hivyo tu, bali imethibitishwa kimajaribio kwamba Moyo wa mwanadamu huathiri uwezo wa kufikiri wa Ubongo, na hivyo uwezo wake wa kimwili wa kukubali, kuelewa na kuhifadhi maarifa. Imethibitishwa pia kuwa Moyo wa mwanadamu huwasiliana na Ubongo na mwili wote wa mwanadamu kwa njia ya neva (kupitia mfumo wa neva - through the nervous system), biophysically (kupitia mawimbi ya Moyo - through pulse waves), biochemically (kupitia homoni fulani - through certain hormones), na umeme (kupitia mawimbi ya nishati - through energetic waves).

Sehemu ya sumakuumeme ya Moyo wa mwanadamu ndio uwanda wenye nguvu zaidi unaozalishwa na mwili wa mwanadamu. Hufunika kila seli katika mwili huo, na kuenea nje katika pande zote hadi katika nafasi inayoizunguka, kama mtoaji muhimu wa habari.

USHIRIAKIANO KATI YA MOYO NA UBONGO

Akili ya Moyo inaweza kuchakata taarifa kuhusu mwili wake na mazingira yake.

Upatanishi wa Moyo wa mwanadamu na Ubongo (Heart and Brain Coherence) uliogunduliwa hivi majuzi na mwanasaikolojia wa Marekani, Paul Pearsall (1998) hali hii inayojulikana kama Upatano wa Moyo na Ubongo (Heart and Brain Coherence) ni ukweli uliothibitishwa, unaothibitisha kwamba shughuli za Moyo wa mwanadamu huathiri ule wa Ubongo, na kwamba Moyo una aina yake ya akili.

Hii hufanyika kupitia "msimbo wa habari wenye nguvu (energetic)" katika mfumo wa mtandao mkubwa wa mishipa ya damu na seli ambazo hutumika kama mfumo wa kukusanya na kusambaza habari za nishati, huitwa "msimbo wa Moyo (heart code)".

Kwenye Qur'ani Tukufu kumelezewa ukweli huu zaidi ya karne 14 zilizopita, huu ni ushuhuda mwengine ulio hai kuwa Qur'an asili yake ni kutoka kwake MwenyeziMungu na ni uthibitisho wa Utume sahihi wa mjumbe mtukufu aliyeupokea.

Suurat Al-A'raaf (7): 179

Na tumeiumbia Jahannamu Majini wengi na Watu. Wana Nyoyo, lakini hawafahamu kwazo. Na wana macho, lakini hawaoni kwayo. Na wana masikio, lakini hawasikii kwayo. Hao ni kama nyama howa, bali wao ni wapotofu zaidi. Hao ndio walio ghafilika.

Kwa hivyo, Mioyo inaweza kuwa na afya au ugonjwa. Mioyo yenye afya (au laini) inaweza kuwa na mtazamo wao wa kibinadamu na usawaziko wa kimantiki, ilhali Mioyo iliyo na magonjwa (au migumu, mawe) inaweza kupoteza wahusika waungwana na wenye utu.            

Msisitizo wa Qur'an juu ya jukumu hili kubwa la Moyo wa mwanadamu - katika maamuzi ya kiakili, kihemko na kiroho, ulifunuliwa zaidi ya karne 14 zilizopita, wakati madaktari wa Moyo na saikolojia wamegundua ukweli kama huo mwanzoni mwa karne ya ishirini na moja.

MOYO WAKO UNA AKILI ZAKE YENYEWE

Imegundulika kuwa Ubongo wako sio kompyuta pekee kwenye mwili wako. Na wala si sehemu ya maamuzi ya msingi katika mwili wako. Ingawa wale wanaofahamu akili ya Moyo hupenda kuuita Moyo kuwa ni “Ubongo wa Pili (Second Brain)".

Miaka kadhaa nyuma, mwaka 2007, timu ya wanasayansi wakiongozwa na Profesa J. Andrew Armour, MD, Ph.D., wa Chuo Kikuu cha Montreal, waligundua Moyo unahifadhi zaidi ya nyuroni 40,000, au neva za hisia. Nyuroni hizi za hisia huunda mtandao wa mawasiliano sawa na tulio nao kwenye Ubongo. Neuron hufafanua seli maalumu inayoweza kuchochewa kwa umeme na kuwasilisha taarifa kwa seli nyingine mwilini. Ingawa hizi zimejulikana kwa muda mrefu kuwepo ndani ya Ubongo na uti wa mgongo, ni jambo la kushangaza kwa kugundulika kwa seli hizi kwenye Moyo.

Tofauti na uko nyuma wanasayansi waliamini kuwa Moyo si chochote ila ni pampu tu, yenye misuli ndani ya vifua vyetu. Ugunduzi huu unatupa ufahamu mpya na muhimu sana kuhusu uwezo wa akili wa Moyo na vilevile kiwango kikubwa cha mawasiliano kilicho kati ya Moyo wetu na miili yetu yote.

MAAJABU YA MOYO

Hadithi chache za kustaajabisha kuhusu uwezo mkubwa wa akili wa Moyo kuweza kuhifadhi kumbukumbu, hata pale Moyo wa mtu unapo pandikizaji kwenye mwili wa mtu mwingine. 

Kuna matukio kadhaa ya kushangaza kabisa yanayohusiana na wagonjwa wa kupandikiza Moyo ambayo yanatulazimisha angalau kukiri akili isiyo na kikomo ya Mioyo yetu.

Mwanamke mmoja aliyepandikizwa Moyo wa mtu mwingine aliwastaajabisha madaktari wake pale alipopata nafuu, alipogundua kuwa alikuwa na hamu kubwa ya kula nyama ya kuku wa kukaanga wa KFC na pilipili hoho.

Hili lilikuwa jambo lisilo la kawaida kwake kwa sababu hakuwahi kutamani au hata kufurahia kula kuku wa kukaanga au pilipili hoho za KFC.

Lakini ajabu tamaa na hamu ilizidi kuwa kubwa tangu afanyiwe upasuaji, na alijua kuwa hamu hii inahusiana na Moyo alioupata. Baada ya kufanya uchunguzi wa kibinafsi, alifanikiwa kujua mfadhili wake alikuwa nani na kuwasiliana na familia yake. 

Wakati wa mazungumzo aliyokuwa nao, walimwambia kwamba vyakula alivyovipenda zaidi marehemu ni nyama ya kuku wa kukaanga wa KFC na pilipili hoho.

Kesi nyingine kubwa iliyo wastaajabisha wengi hadi sasa ni kuhusu msichana mwenye umri wa miaka 8 ambaye alipokea Moyo wa msichana wa miaka 10 ambaye alikuwa ameuawa kikatili. Msichana huyo mwenye umri wa miaka 8 alianza kuota ndoto mbaya za kutisha za mara kwa mara tangu alipopokea Moyo wake mpya.

Msichana huyo wa miaka 8, alikuwa akiota mara kwa mara akifukuzwa na mwanaume mmoja aliyekuwa akimfukuza msituni na kumuumiza. Jinamizi hilo lilimsumbua sana mpaka kupelekea maamuzi ya yeye kupelekwa kwa mshauri nasaha ambaye alihitimisha kuwa binti yule alikuwa akielezea tukio halisi, lililowahi kutokea. 

Mshauri nasaha yule baada ya kuelezwa kuwa matukio hayo ya ndoto za kukimbizwa yamejitokeza baada ya kufanyiwa upasuaji wa Moyo na kuwekwa Moyo wa msichana mwingine mwenye umri wa miaka 10. Ndipo akawashauri wazazi wa yule mtoto waende kwenye vyombo vya sheria (Polisi), na uko polisi msichana akaelezea tukio analo liona kwenye ndoto zake za mara kwa mara kama vile; mahali na wakati wa tukio, mavazi na hata maneno ambayo msichana aliyasikia kwenye ndoto zile za kutisha. Maneno ambayo mtu yule muuwaji alikuwa akiyasema alipokuwa akimumiza. 

Taarifa za msichana zilipelekea muuwaji akamatwe na kutiwa hatiani. Hii ilikuja kubainika kuwa hayo maneno ndio kumbukumbu ya mwisho ya tukio halisi la masaibu yaliyompata yule mtoto wa miaka 10, muuaji yule baada ya kuhojiwa alikiri na kuthibitisha kuwa ni kweli yeye ndio muuwaji wa yule msichana wa miaka 10.

Hii inatuonyesha kwamba Moyo wa msichana huyu mdogo ulihifadhi kumbukumbu ya shambulio lake na kuipitisha kwa mpokeaji wa Moyo wake, ambayo hatimaye ilipelekea kupatikana kwa muuwaji.

Kisa kingine cha kustaajabisha ambacho kimeripotiwa kinahusu mwanamke mmoja shoga (Msagaji) ambaye aliupenda ushoga na kuukumbatia. Ni Mwanamke ambaye alipenda sana kuwa Mwanaume kuliko uanamke wake katika maisha yake. 

Mwanamke huyo alipata bahati ya kupandikizwa Moyo wa mtu mwingine ambaye hakuwa shoga. 

Mfadhili wake alikuwa mwanamke, mwanamke aliyeupenda uwanamke wake na alikuwa anapenda kula mboga (Vegetarian) maishani mwake. 

Baada ya kuupokea Moyo wake mpya, alijikuta akichukizwa na ulaji wa nyama na hakupenda tena kufanya ngono za jinsia moja na wanawake wenzake. Alianza kuukubali zaidi uanamke wake na kuanza kupenda wanaume wenye mvuto wa kimapenzi, jambo ambalo hakuwahi kulihisi katika maisha yake yote. Hatimaye aliendelea kuwa vejitelian na akaja kuolewa na mwanamume.

Kinyume na sayansi ya zamani, Moyo wako ni zaidi ya chombo kisichochoka, kinachosukuma damu. Moyo wako una uwezo wa ajabu wa kufikiri, kuhisi, kujifunza na kukumbuka bila kutegemea Ubongo wako.

NYONGEZA

  • • Moyo una mfumo wake wa neva unaojitegemea, unaojumuisha nyuroni zaidi ya 40,000.
  • • Sehemu ya sumakuumeme ya moyo ndio uwanja wenye nishati zaidi unaozalishwa na mwili wako, na huangaza futi kadhaa nje ya mwili wako.
  • • Mapigo ya moyo wako, si kusukuma damu tu, bali ni moja ya njia ya kusambaza mtiririko wa nishati kwa kila seli.
  • • Moyo hukupa mwongozo wa kihemko na angavu kukusaidia kuelekeza maisha yako.
  • • Hisia za moyo hutoa maamuzi ya msingi kama vile, upendo, shukrani, huruma n.k na pia udhibiti maamuzi aidha kupigana au kukimbia.
  • • Midundo ya Moyo wako inaakisiwa katika hali zako za kihisia. Hisia hasi kama vile woga, hasira, na uhasama huunda tofauti isiyo ya kawaida na isiyo ya kawaida ya mapigo ya moyo (tofauti nzuri katika muda kati ya mapigo ya moyo). Hisia chanya huunda mpangilio ulioboreshwa katika midundo ya moyo.
  • • Moyo ndio kisisitizo kikuu cha mwili, mdundo wake huvuta mifumo yote ya mwili kuwa katika hali ya kujizuia au kusawazisha.
  • • Hali nzuri za kihisia zina athari ya kusawazisha kwenye mfumo wa neva kwa kuimarisha kinga, kuimarisha kazi ya homoni, na kuboresha kazi ya ubongo.

0 comments:

Post a Comment

Je Una Nasaha zozote Kuhusiana na Makala hii?

RAMADHAN KARIM

Read

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!