JE, NI MASLAHI BINAFSI, UKOSEFU WA MSIMAMO AU
KUPUUZA HISTORIA YA MAUAJI TANZANIA?
Kuhama
chama si dhambi. Dhambi ni kuhama misimamo, kuhama ukweli, na kuhama
dhamana kwa wananchi. Historia ya mauaji inatukumbusha: cheo ni
dhamana, si kinga. Mwanasiasa anayepuuza historia hii, leo akisifia,
kesho akilaani, huyo anapigania tumbo lake tu.
Wanasiasa
wa Tanzania wanapaswa kutambua kuwa historia itawahukumu vikali.
Kitendo cha kuweka mbele maslahi ya matumbo yao na kuwa tayari
kugeuka geuka kiitikadi kinazidi kuchelewesha upatikanaji wa Katiba
Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi, vitu ambavyo vingemaliza kabisa
mzunguko huu wa ukatili na mauaji kila msimu wa uchaguzi. Bila kuwa
na viongozi wenye msimamo thabiti (kama ule wa uwajibikaji wa Ali
Hassan Mwinyi wa mwaka 1976), siasa za Tanzania zitabaki kuwa
biashara ya watu wachache, huku raia wa kawaida wakiendelea kuwa
wahanga wa upepo wa kisiasa.
---
1.
UTANGULIZI:
“SIASA
HAINA ADUI WA KUDUMU” – KAULI AU KISINGIZIO?
HAMAHAMA
YA WANASIASA: Katika siasa za Tanzania hasa vyama vya siasa
viliporuhusiwa au kurejeshwa tena, kumekuwa na wimbi la wanasiasa
kuhama vyama, leo yupo chama fulani, kesho anarudi au kuhamia
kingine. Swali kuu linabaki: je, hii ni ishara ya demokrasia yenye
afya au ni dalili ya kukosekana kwa misingi, msimamo na uwajibikaji
wa kisiasa?
Swali
la Msingi: Wanatafuta Nini?
Ni
kutafuta maslahi binafsi (matumbo), ukosefu wa msimamo thabiti, au
kupuuza historia ya mauaji na ukandamizaji wa kiutawala nchini?
Mjadala
huu hauwezi kukamilika bila kuangalia historia ya nchi, hasa matukio
mazito ya kiusalama na mauaji ambayo yalipaswa kuwa somo kwa
wanasiasa wa Tanzania ili kujenga misimamo thabiti.
SIASA ZA
KUHAMAHAMA VYAMA: UHURU AU MASLAHI?
Kihalisia,
katiba na sheria za vyama vya siasa zinamruhusu mwanasiasa kuchagua
chama anachotaka. Hata hivyo, changamoto ipo kwenye nia na muda wa
maamuzi hayo.
Kwa
mujibu wa wachambuzi, wanasiasa wanaohama wamegawanyika makundi
mawili:
WENYE
MISINGI NA ITIKADI: Wanahamia chama chenye maadili wanayoamini. Ni
Wanasiasa wachache sana, huhama kwa sababu za sera na mwelekeo.
WAPENDA
MASLAHI BINAFSI: “Popote panapo maslahi watakwenda”. Hawa ndio
waliozua msemo “Siasa Haina Adui wa Kudumu” kauli ambayo kwangu
mimi naiona kama upuuzi na ulaghai.
Hawa
ni wenye siasa za matumbo; hutanguliza maslahi binafsi kuliko maslahi
ya wananchi. Hawa ndio wanaoleta mashaka makubwa kwa jamii.
Wanapokuwa nje ya mfumo, huikosoa serikali kwa nguvu zote. Lakini
wanapopata nafasi ndani ya mfumo huo huo:
Tatizo
linakuja pale mwanasiasa anapokuwa serikalini: anasifia mfumo.
Akiondolewa au kumaliza muda, ghafla anakuwa mkosoaji mkubwa. Hii
inazua maswali: je walikuwa wanaficha ukweli wakiwa madarakani? Au
walikuwa wanakula keki kimyakimya?
2. HISTORIA YA
MAUAJI YA KISIASA TANZANIA:
Na
Athari Zake Kisiasa, Kwa Nini Inapaswa Kukumbukwa.
Kabla
ya kumhukumu mwanasiasa anayehama, ni muhimu kuweka mizani ya
historia ya damu iliyomwagika. Historia hii ndiyo inayopaswa
kutengeneza misimamo ya viongozi.
2.1.
Mauaji ya Shinyanga 1976 na Kujiuzulu kwa Ali Hassan Mwinyi.
Julai
1976, yalitokea mauaji mkoani Shinyanga. Ali Hassan Mwinyi, akiwa
Waziri wa Mambo ya Ndani, alimuandikia Rais Mwalimu Nyerere barua ya
kujiuzulu uwaziri. Alisema “Hakuna
sababu ya kiongozi kujiuzulu baada ya kutokea mauaji” lakini
yeye aliona ni wajibu kuwajibika.
Uamuzi
huo ulimjengea heshima na baadaye mwaka 1985 akawa Rais wa Awamu ya
Pili.
Somo
hapa tunaona mfano wa uwajibikaji wa kisiasa, jambo ambalo siku hizi
lhalipo. Leo, viongozi wangapi wako tayari kuwajibika mauaji
yanapotokea?
2.2
Mauaji ya Mwembechai, 13 Februari 1998
Siku
ya Ijumaa, 13 Februari 1998, polisi wa FFU walifyatua risasi kwa
waumini wa Kiislamu Msikiti wa Mwembechai, Dar es Salaam. Angalau
watu wanne waliuawa. Tukio lilitokana na mchungaji wa Kikatoliki
kudai Waislamu walikuwa wakimkejeli Yesu, madai yaliyothibitika kuwa
ya uongo.
Waziri
wa wakati huo wa Mambo ya Ndani, Ali Ameir, alisema hali hiyo ilikuwa
moja ya changamoto kubwa alizokumbana nayo.
Hili
lilizua:
Maswali
juu ya matumizi ya nguvu za dola
Hofu
ya mgawanyiko wa kijamii
Wito
wa uwajibikaji wa viongozi
Tukio
hili liliibua maswali kuhusu uhuru wa dini na matumizi ya nguvu
kupita kiasi na vyombo vya usalama.
Lakini,
je, wanasiasa wa leo wanajifunza nini kutoka hapa? Au wanalitumia tu
kama silaha ya kisiasa wanapokuwa nje ya madaraka?
Muda
baadae, Msomi ambaye hapendi kuitwa Profesa, aliekuwa mhadhiri
muandamizi Udsm, Professor Hamza Mustafa Njozi, akaandika kitabu
"Mwembechai
Killings and the Political Future of Tanzania"
ni kazi inayochunguza mauaji ya Mwembechai ya mwaka 1998 jijini Dar
es Salaam na kuangazia athari zake pana kwa haki, demokrasia, na
utulivu wa kisiasa nchini Tanzania.
Kitabu
kilipigwa marufuku kuingia nchini wakati wa Rais Mkapa.
Serikali
ilikataa uchunguzi huru na ikapiga marufuku mkutano wa wanawake wa
Kiislamu waliotaka kuzungumza unyanyasaji waliopata rumande.
Mwembechai ikawa alama ya ubaguzi wa kidini na matumizi mabaya ya
dola.
2.3 OPERESHENI
MKIRU - (Mkuranga, Kibiti, Rufiji) 2013-2017
MKIRU
ni kifupisho cha Mkuranga,
Kibiti NA Rufiji.
Hayo ni maeneo yaliyokumbwa na mauaji ya polisi na viongozi wa
serikali kuanzia 2013.
Eneo
la Pwani ya Tanzania, lilishuhudia mfululizo wa mauaji ya askari
polisi na raia. Serikali ilianzisha Operesheni MKIRU ili kukabiliana
na kile kilichoitwa ugaidi au uhalifu uliopangwa. Operesheni hii
ilitumia ujasusi mkubwa na ilifanikiwa kupunguza matukio hayo.
Hata
hivyo, ilizua madai ya ukiukaji wa haki za binadamu.
Chanzo
kikuu kilichotajwa:
Chuki
za wananchi dhidi ya polisi: 23
Januari 2013, mkazi wa Kibiti alifariki Muhimbili kwa madai ya
kupigwa na polisi. Wananchi walifunga Barabara ya Kilwa kwa zaidi ya
saa 3 na kuchoma kituo cha polisi.
Unyanyasaji
wa kiuchumi:
Ripoti ya Mwananchi Mei 26, 2017 ilieleza kuwa vijana wa MKIRU
wanategemea mkaa, magogo, mazao, lakini wananyanyaswa na mamlaka,
maliasili, mgambo na polisi.
Hadi
leo, dhana 4 zinazunguka MKIRU: Ugaidi, Chuki za Kisiasa, Chuki Dhidi
ya Polisi, au Uhalifu wa Kawaida.
Matukio
haya:
Lakini
bado, hakuna mjadala wa kina unaoongozwa na wanasiasa wenye msimamo,
wengi huongea kwa msimu.
2.4 MAUAJI YA
ZANZIBAR KILA UCHAGUZI.
(Kuanzia
Mwaka 1995, 2000, 2005, Hadi 2021).
Zanzibar
ina historia ndefu ya damu wakati wa uchaguzi:
29
Oktoba 2000: Uchaguzi
ulivurugwa. Waangalizi wa Jumuiya ya Madola, OAU, SADC walisema
ulikuwa na dosari kiasi cha kutokuwa na hadhi ya kuitwa uchaguzi.
27
Januari 2001:
Polisi waliwaua waandamanaji wa CUF. Serikali ilisema waliuawa 23,
CUF walisema 67. Human Rights Watch ilithibitisha angalau 35 na
zaidi ya 600 kujeruhiwa. Zaidi ya 2000 walikimbilia Kenya kama
wakimbizi.
2020-2025:
Vikundi
vya “Janjawid” na vikosi kazi vimedaiwa kutumika kuumiza
wapinzani. Haji Omar Kheir, Mshauri wa Rais tangu 2023, ametajwa
majukwaani na Maalim Seif kuwa muasisi wa vikundi hivyo.
Historia
ya chaguzi za Zanzibar imekuwa ikihusishwa na:
Vurugu.
Mauaji.
Migogoro
ya kisiasa.
Haya
si mambo mapya, lakini swali ni:
Kwa
nini bado yanajirudia kila uchaguzi?
2.5 TUKIO LA 29
OKTOBA 2025.
Hadi
kufikia nyakati za hivi karibuni, ikiwemo matukio mabaya ya mfululizo
wa utekaji, upotezwaji wa watu, na vifo vya wanaharakati pamoja na
viongozi wa kisiasa wa upinzani (kama vile mauaji ya wanasiasa wa
Upinzani, na wengine), damu inaendelea kumwagika. Wananchi wanapoteza
maisha wakiamini wanapigania mfumo bora wa maisha, huku wanasiasa
wakichukulia harakati hizo kama mtaji wa biashara zao binafsi.
Uchaguzi
Mkuu wa 29 Oktoba 2025 ulifuatiwa na ukandamizaji mkubwa. Ofisi ya
Haki za Binadamu ya UN iliripoti:
Mamia
waliuawa, idadi isiyojulikana kujeruhiwa au kukamatwa.
Zaidi
ya 150 walikamatwa tangu siku ya kura, wengi wakiwa watoto,
wakishtakiwa kwa uhaini.
Inasemekana
miili ilichukuliwa na vyombo vya dola na kupelekwa sehemu
zisizojulikana ili kuficha ushahidi.
Miundombinu
na mali za watu binafsi ziliharibiwa, kupelekea wengi kupata hasara
na hata kufirisika.
Mashahidi
walisema askari walifyatua risasi za moto moja kwa moja. Viongozi wa
upinzani na makundi ya haki wanasema vifo ni “mamia hadi zaidi ya
elfu”, wengi wakiwa vijana, wanawake, watoto. Asilimia 95 ya
waathirika walipigwa risasi kichwani au kifuani kwa karibu, kuashiria
“nia ya kuua sio kutawanya”.
Mtandao
ulizimwa, vyombo vya habari vikadhibitiwa. UN ilitaka uchunguzi huru
na kuachiliwa kwa Tundu Lissu na wengine.
Hali
hii imepelekea kujiuliza mambo haya matatu:
Lakini
badala ya kujenga hoja za pamoja, wanasiasa wengi wamegawanyika
kulingana na maslahi yao binafsi.
3. KWA NINI
WANASIASA “NJE YA MFUMO” HAWAJUMLISHI KUPATA MAJIBU?
Wengi
wanaopinga serikali wakati wako nje ya madaraka, wanapopata vyeo huwa
kimya au wanashiriki katika mfumo huo huo.
Ukosefu
wa Uwajibikaji wa Kitaasisi: Tangu Mwinyi ajiuzulu 1976, ni viongozi
wachache wamewajibika. Mauaji ya Mwembechai 1998, MKIRU 2017,
Zanzibar 2001 na 2025, hakuna ripoti ya wazi ya serikali wala hatua
kwa wahusika. Hii inafanya “nje ya mfumo” wasiamini mfumo utatoa
haki.
Matumizi
ya Dola Kulinda Maslahi: Historia inaonyesha polisi na vyombo vya
usalama vikitumika kukandamiza upinzani. Hivyo mwanasiasa akitoka
nje, anakuwa hana ulinzi.
“Maslahi
ya Tumbo” vs Msimamo: Wapo wanaosubiri nafasi. Wakiwa nje wanasema
serikali ni mbaya. Wakipewa uteuzi, wananyamaza. Hii ni “undumila
kuwili na Ubarakala” – unafiki wa kisiasa. Lakini pia wapo
wanaohofia uhai wao. Bila ulinzi wa kisheria, kusema ukweli ukiwa
ndani ni hatari.
3.1. SIASA ZA KUHAMAHAMA VYAMA: UHURU
AU MASLAHI?
Kihalisia,
katiba na sheria za vyama vya siasa zinamruhusu mwanasiasa kuchagua
chama anachotaka. Hata hivyo, changamoto ipo kwenye nia na muda wa
maamuzi hayo.
Kwanini
hawaunganishi dots (hawajumlishi, hawatoi wala kuzidisha, sembuse
kugawanya) kupata majibu?
Wanasiasa
wa Tanzania wanajua fika historia ya mauaji ya Shinyanga,
Mwembechai, Zanzibar, na utekaji wa sasa. Wanajua kuwa tatizo ni
mfumo wa kiutawala (Structural Problem) unaolinda madaraka ya chama
kimoja na kuminya haki. Hata hivyo, hawataki kujumlisha matukio haya
ili kujenga msimamo imara wa muda mrefu kwa sababu msimamo
unagharimu. Kupigania mfumo wa haki kunahitaji kujitoa mhanga, jambo
ambalo wanasiasa wengi hawapo tayari kulifanya pindi fursa ya "kula"
inapojitokeza. Wanapigania maslahi ya matumbo yao na familia zao.
Unafiki
wa kutosusia nyadhifa za kiserikaliHili ni swali la msingi sana:
Kwanini mwanasiasa anayejinasibu kuwa upande wa wananchi
akichaguliwa au kuteuliwa kwenye nafasi ya kiserikali (kama ubunge,
uwaziri, au ubalozi) hawakatai?
Wanapokuwa
ndani ya mfumo, wananyamaza kimya kabisa. Hawazungumzii mauaji,
hawazungumzii utekaji, na wanatetea bajeti na sera mbovu.
Wanajifanya
kuona serikali ni mbaya na ina ukatili pale tu wanapomaliza muda wao
au wanapoondolewa kwenye vyeo vyao (Political Rejection). Huu ni
uthibitisho tosha kwamba hawakuwa na uchungu na nchi, bali walikuwa
na uchungu wa kupoteza fursa ya kufaidika na mfumo.
"Mwanasiasa
anayelalamika kuwa mfumo ni mbaya baada ya kufukuzwa kazi,
halalamikii mfumo, analalamikia kukatwa kwa mirija yake ya ugali."
3.2 AINA TATU
ZINAZO PELEKEA WANASIASA KUHAMAHAMA VYAMA:
Wenye
Misingi ya Kiitikadi:
Wachache sana, huhama kwa sababu za sera na mwelekeo.
Wanaotafuta
Nafasi:
Uhama pale wanaponyimwa uteuzi au mamlaka. Hawa ndio wale siasa za
tumbo (Mslahi Binafsi). Hutanguliza maslahi binafsi kuliko maslahi
ya wananchi. Wengine hubadili vyama ili kupata nafasi za kiserikali,
mikataba, au ulinzi.
Ukosefu
wa Taasisi Thabiti za Vyama: Vyama
vingi vinategemea watu binafsi badala ya msimamo wa kiitikadi.
Kupuuza
Historia:
Wanasiasa wachache hujenga misimamo thabiti kuhusu mauaji ya
kihistoria (Shinyanga,
Mwembechai, MKIRU, Zanzibar) ili
kuzuia kurudiwa. Badala yake, wengi hujikita katika siasa za Matukio
ya sasa kwa faida binafsi.
3.3 MIFANO HAI YA VIONGOZI
WALIOHAMAHAMA.
Wabunge
na madiwani wengi wametoka vyama vya upinzani (kama CHADEMA, CUF) na
kujiunga na CCM wakati wa mabadiliko ya uongozi, wakidai “kuunga
mkono maendeleo.”
Baadhi
ya viongozi wa zamani wa upinzani wamechukua nyadhifa serikalini na
kuacha kuikosoa serikali kwa ukali walioonyesha awali. Hii inaweza
kuashiria undumilakuwili, kuwa na sura mbili kulingana na nafasi.
Hizi
ndizo sababu nizionazo zinazoleta mashaka makubwa kwa jamii.
Wanasiasa wanapokuwa nje ya mfumo, huikosoa serikali kwa nguvu zote.
Lakini wanapopata nafasi ndani ya mfumo huo huo:
Hii
inazua swali:
Je,
tatizo ni nini?
3.4
CHART
|
Jina
la Kiongozi
|
Kuhama/Kubadili
Msimamo
|
Muktadha
na Sababu
|
|
Edward
Lowassa
|
Kutoka
CCM kwenda CHADEMA (2015), kisha kurudi CCM (2019).
|
Baada
ya jina lake kukatwa CCM mwaka 2015, alihamia upinzani akidai
mfumo wa CCM ni mbaya na haufai. Alikaribishwa na CHADEMA kama
"shujaa". Baada ya uchaguzi kupita na upepo kubadilika
chini ya Hayati Magufuli, alirejea tena CCM na kusifu kazi ya
chama hicho.
|
|
Dr.
Willibrod Slaa
|
Kutoka
CHADEMA kwenda Diplomasia (CCM), kisha kurudi upinzani.
|
Alikuwa
katibu mkuu wa CHADEMA na nembo ya mapambano dhidi ya ufisadi.
Mwaka 2015 alijiondoa CHADEMA kupinga ujio wa Lowassa. Na hata
kuongeza misumari na kuituhumu CHDEMA kuwa inateka wanachama wake
wenyewe. Baadaye aliteuliwa na serikali ya CCM kuwa Balozi. Baada
ya kustaafu ubalozi, amerudi tena kwenye msimamo wa kuikosoa
vikali serikali kupitia majukwaa ya kiraia.
|
|
Lazaro
Nyalandu
|
Kutoka
CCM kwenda CHADEMA, kisha kurudi CCM.
|
Alikuwa
Waziri ndani ya CCM, akahama na kwenda upinzani akidai mfumo
unaminya demokrasia. Baada ya mambo kuwa magumu kisiasa, alirejea
tena CCM akidai anaunga mkono juhudi za mwenyekiti.
|
|
Prof.
Kitila Mkumbo
|
Kutoka
ACT-Wazalendo kwenda CCM.
|
Alikuwa
mmoja wa waasisi wa ACT-Wazalendo na mkosoaji mkubwa wa kiuchumi
wa serikali ya CCM. Baada ya kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara
ya Maji na Rais Magufuli, alihamia rasmi CCM na sasa ni Waziri na
mtetezi mkubwa wa mfumo ule ule aliokuwa akiukosoa.
|
|
Mch.
Peter Simon Msigwa
|
Kutoka
CHADEMA kwenda CCM (Juni 2024), kisha kurudi
CHADEMA (Mei 2026)
|
Baada
ya kushindwa kwenye uchaguzi wa Kanda ya Nyasa ndani ya CHADEMA
dhidi ya Tundu Lissu, alitangaza kukihama chama hicho kwa hasira
na kujiunga na CCM, huku akimshambulia vikali Freeman Mbowe kwa
madai ya udikteta. Hata hivyo, baada ya kukaa CCM kwa takriban
miaka miwili na kuambulia patupu kwenye kura za maoni za kuelekea
uchaguzi, mnamo Mei
2026 ametangaza rasmi kurejea CHADEMA akidai
"nimechoka kuishi kwa huzuni" na kuwaomba radhi
Watanzania.
|
Maneno ya Peter
Msigwa Wakati wa Kuhama.
Uhamaji wa
Mchungaji Peter Msigwa kwenda CCM uliambatana na kauli nzito
zilizowaacha wananchi na maswali mengi kuhusu msimamo wake wa
kiitikadi na "unabii" wa kisiasa aliokuwa akihubiri huko
nyuma.
1. Kauli ya "Bata
na Tai" (Kujitetea Kuhama CHADEMA)
Alipokuwa akihojiwa
na vyombo vya habari kuelezea sababu ya kukimbilia CCM baada ya
kushindwa uchaguzi wa ndani CHADEMA, Msigwa alitoa mfano wa ndege
akisema:
"Mimi
ni mtu wa kusema haki, mimi ni mtu wa kunyoosha maelezo, mtu wa
kusema ukweli. Sasa kuna vitu ambavyo naona nikiwa upande huu
[CHADEMA], ile umimi inashindwa. Naanza
kuwa bata wakati natakiwa niwe eagle (tai).
Sasa nikaona isiwe tabu..."
Kauli hii ilitumiwa
na wakosoaji wake kuonyesha jinsi alivyokuwa akijitwika ukuu wa "Tai"
(ndege anayeona mbali na mwenye nguvu), huku akidhalilisha taasisi na
wanachama alioacha nyuma kama "Bata".
2. Kumlipua
Freeman Mbowe na Kudai CHADEMA Hakuna Demokrasia
Wakati anapokelewa
na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Samia Suluhu Hassan mnamo Juni 2024,
Msigwa hakusita kurusha makombora kwa viongozi wake wa zamani.
Alimshambulia waziwazi Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, kwa
kumlinganisha na madikteta wa nchi za jirani:
Alidai
kuwa CHADEMA imepoteza mwelekeo, haina demokrasia ya kweli, na
inafanya "siasa za uongo". Alidai kuwa ndani ya chama hicho
hakuna anayetakiwa kuhoji mamlaka ya Mwenyekiti na yeyote anayejaribu
kufanya hivyo anakatwa mabawa.
3. Kugeuka na
Kusifu Mfumo wa CCM
Ndani ya kipindi
chake kifupi akiwa CCM, msimamo wa Msigwa ulibadilika kwa digrii 180.
Yule Mchungaji aliyekuwa akipiga kelele majukwaani akilaani ukatili
wa serikali ya CCM, mauaji ya Zanzibar, na ukandamizaji, alianza
kusikika kwenye mikutano ya kampeni (kama kule Ismani mkoani Iringa)
akisema:
"Tanzania
ipo salama chini ya Chama Cha Mapinduzi. Upinzani hawana sera za
ukombozi, CCM pekee ndicho chama chenye uwezo wa kuongoza na
kuwaletea wananchi maendeleo."
Ukweli wa Siasa za
"Matumbo": Msigwa Katupwa Kabatini na Kurudi CHADEMA (Mei
2026)
Mchezo huu wa
kuigiza wa Mchungaji Msigwa umekuja kuthibitisha kwa vitendo hoja kuu
ya makala yetu, kwamba wanasiasa
wanatafuta maslahi ya matumbo yao na fursa za madaraka.
Baada ya kuhamia
CCM kwa mbwembwe na kugeuka kuwa "chawa" wa kusifu kila
kitu, Msigwa aliamini angetunziwa heshima yake na kupitishwa kugombea
Ubunge wa Iringa Mjini kupitia tiketi ya CCM. Hata hivyo, mfumo wa
CCM ulimtumia kama "karai" la kupigia propaganda na kisha
kumtupa kando. Kwenye mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM kuelekea
Uchaguzi Mkuu, jina la Msigwa liliangukia pua na halikuwemo hata
kwenye majina matatu ya juu ya wanachama waliopendekezwa na wajumbe.
Baada ya kuona
amewekwa "kabatini" na kupoteza umaarufu wote wa kisiasa
mbele ya jamii, mnamo Mei
2026, Mchungaji Msigwa
ameamua "kulamba matapishi yake" na kutangaza kurejea
CHADEMA kwa aibu, akitoa kauli mpya inayovunja moyo:
"Nimechoka
kuishi kwa huzuni, Watanzania naomba mnisamehe..."
Huu ni uthibitisho
mwingine hai kuwa wanasiasa hawa hawana chembe ya msimamo wa
kiitikadi; upepo wa maslahi binafsi ukivuma upande wa mashariki
wanakuwa "Tai wa kijani", upepo ukiwakataa wanarudi upande
wa magharibi kuwa "Bata wa bluu", huku damu ya wananchi
wanaouawa kwenye harakati za kulinda vyama hivyo ikiendelea kupuuzwa.
Wimbo huu wa Peter
Msigwa atangaza kurudi CHADEMA
unaonyesha video ya tukio la hivi karibuni ambapo mwanasiasa huyo
anaomba radhi hadharani na kutangaza rasmi kurejea chama chake cha
zamani baada ya safari yake ya kisiasa ndani ya CCM kukwama.
3.5 BILA KUWAHUKUMU, TUANGALIE MIFANO
YA TABIA:
Kundi
la “Waliokurupuka 2015-2020”: Wanasiasa kadhaa walihama kutoka
upinzani kwenda CCM wakati wa utawala wa Rais Magufuli. Hoja yao:
“utawala umekubalika”. Wakosoaji wanasema walitafuta ulinzi
baada ya kubanwa.
Kundi
la “Waliotoka CCM 2022-2024”: Baadhi ya wabunge na madiwani
walihamia upinzani baada ya kukosa teuzi au kura za maoni. Walidai
“wanataka mabadiliko”. Lakini walipokuwa ndani, hawakuyasema.
Zanzibar:
Haji Omar Kheir alishindwa uchaguzi Tumbatu, akalia kwenye mtumbwi.
Baadaye ZEC ikamtangaza mshindi. Akiwa Waziri wa vikosi, vikundi vya
kihalifu vilishamiri. Leo ni Mshauri wa Rais. Mfano wa jinsi mfumo
unavyoweza kutumika.
3.6 TATIZO KUBWA: Ukosefu wa Msimamo
wa Kisiasa
Wanasiasa
wengi:
Hawajengi
misingi ya kudumu ya sera.
Wanabadilika
kulingana na upepo wa kisiasa.
Wanashindwa
kuunganisha nguvu wanapokuwa nje ya mfumo.
Badala
ya:
Wanageuka
kuwa:
“Wapinzani
wa muda na watawala wa muda”
4. JE, NI UNDUMILA
KUWILI NA UBARAKALA?
Ndiyo,
kama kigezo ni “unasema
nini ukiwa ndani dhidi ya ukiwa nje”.
Lakini pia ni swali la “mazingira”. Mfumo usio na uwajibikaji
unazalisha wanafiki na wanasiasa tumbo, wenye kujipendekeza, kwani
ukweli ni gharama.
Kwa
kuangalia mienendo:
Mwanasiasa
anapokuwa nje ya mfumo: Anaona mfumo ni mbaya.
Akiingia
ndani ya mfumo: Anakwa karambishwa asali, Ananyamaza.
Akitoka/kufukuzwa:
Anarudia ukosoaji ule ule.
Hii
ni ishara ya:
Kukosa
uadilifu wa kisiasa.
Kukosa
ujasiri wa kusimamia ukweli.
Kuweka
mbele maslahi binafsi kuliko taifa.
5. HITIMISHO: Nini
Kifanyike?
Siasa
za bendera kufuata upepo (Siasa Maslahi) ni usaliti mkubwa kwa damu
ya Watanzania waliopoteza maisha huko Shinyanga, Mwembechai, Pemba,
Unguja, na katika barabara za Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla,
kupitia utekaji na mauaji ya kisiasa.
Wanasiasa
wa Tanzania wanapaswa kutambua kuwa historia itawahukumu vikali.
Kitendo cha kuweka mbele maslahi ya matumbo yao na kuwa tayari
kugeuka geuka kiitikadi kinazidi kuchelewesha upatikanaji wa Katiba
Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi, vitu ambavyo vingemaliza kabisa
mzunguko huu wa ukatili na mauaji kila msimu wa uchaguzi. Bila kuwa
na viongozi wenye msimamo thabiti (kama ule wa uwajibikaji wa Ali
Hassan Mwinyi wa mwaka 1976), siasa za Tanzania zitabaki kuwa
biashara ya watu wachache, huku raia wa kawaida wakiendelea kuwa
wahanga wa upepo wa kisiasa.
5.1 TUNAWAJIBIKA:
KUKUMBUKA
HISTORIA:
Shinyanga, Mwembechai, MKIRU, Zanzibar, 29 Oktoba 2025 – damu hizi
ni dira. Mwanasiasa asiyejifunza historia atairudia.
UWAJIBIKAJI
WA LAZIMA:
Kama Mwinyi alivyojiuzulu 1976, tunahitaji utamaduni ambapo waziri,
IGP, RPC anawajibika mauaji yakitokea.
TUME
HURU ZA UCHUNGUZI:
UN imeitaka Tanzania kuchunguza mauaji ya 2025. Bunge linapaswa
kuanzisha tume huru kwa Mwembechai, MKIRU, na Zanzibar.
KATIBA
MPYA: Ili
kuzuia wanasiasa kutumia mianya ya “siasa haina adui wa kudumu”,
tunahitaji katiba inayozuia wabunge kuhama vyama bila kurudi kwa
wananchi.
WANANCHI
WAWE MAKINI:
Wasiangalie maneno bali matendo.
Vyama
vijenge itikadi:
Siasa isiwe ya mtu binafsi.
Historia
ya kweli ya Tanzania, ifundishwe, ili makosa yasirudiwe.
6. MWISHO:
Kuhama
chama si dhambi. Dhambi ni kuhama misimamo, kuhama ukweli, na kuhama
dhamana kwa wananchi. Historia ya mauaji inatukumbusha: cheo ni
dhamana, si kinga. Mwanasiasa anayepuuza historia hii, leo akisifia,
kesho akilaani, huyo anapigania tumbo lake tu.
Jamii
iulize: Kiongozi
wako alisema nini kuhusu MKIRU akiwa Mkuu wa Wilaya au mkoa au hata
ubalozi? Alisema nini kuhusu mauwaji ya kule Zanzibar na 29 Oktoba
2025 akiwa na cheo? Majibu yake ndiyo kipimo cha msimamo wake.
Wajibu
wetu kama raia ni kudai uwajibikaji na kuelimishana ili siasa ziwe za
maendeleo, si za faida binafsi.
Na
kama historia ya mauaji na matukio ya kiusalama haijawafanya raia na
wanasiasa kujifunza, basi swali linabaki wazi:
JE,
WANATUMIKIA NCHI… AU WANAITUMIA NCHI?