Friday 9 September 2022

KWA NINI NDOA HAZIDUMU

· Je, Kuna Haja ya Kuhuisha Mafunzo ya Jando na Unyago?

· Dar Peke Yake Kuna Wastani wa Ndoa 360 Zinavunjika Kila Mwezi.

· Kuongezeka kwa Tabia za Ushoga Katika Jamii.

Hivi karibuni, tumemsikia Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii akisema kuwa kuna haja ya kuchukua hatua na kutafuta kwa kina chanzo cha kuvunjika kwa ndoa nyingi nchini.

Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, ndugu Stanslaus Nyongo, aliyasema hayo siku ya Jumatatu mwezi wa Septemba tarehe 5, 2022 baada ya kukutana na wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia na makundi Maalum.

Dar es Salaam pekee yake zaidi ya ndoa 360 kwa mwezi zinavunjika, ni wastani wa ndoa 12 zinafunjika kila siku.

Hili linaweza kuwa linachangiwa na sababu nyingi kutoka kwa wanandoa wenyewe. Lakini kuna vitu ambavyo tukiviangalia tunajua kuwa ni moja ya sababu zinazopelekea ndoa na mahusiano mengi kuweza kuvunjika.

Wanandoa wengi sasa hivi wanashindwa kuishi maisha ya ndoa, wengi wao wamekuwa wanaharakati zaidi katika ndoa kuliko kuwa walezi, hali ambayo imesababisha migogoro na kuvunjika kwa ndoa nyingi, jambo hili linaathiri ustawi wa familia, maisha, ufanisi katika utendaji kazi.

Watu wengi wanaingia katika ndoa bila kupata elimu na mafunzo ya kutosha kuhusu maisha ya ndoa, haswa kwa kupotea kwa mafundisho ya kijadi ya Jando na Unyago kwa wavulana na wasichana waliobaleheka.

Watu wengi wanaishi kwenye ndoa au mahusiano kusogeza tu siku, ilimradi kunakucha. Ndoa nyingi kwa sasa zimekosa ushirikiano katika kutoa maamuzi ya pamoja yatakayoweza kuwasaidia kujenga familia bora na maisha mazuri ya sasa na ya baadaye.

Inashangaza sana kuona watu wanaoishi pamoja kila mmoja ana mipango na mikakati ya maisha yake. Huyu anawaza kufanya hivi, yule anawaza kufanya vingine na awaambiani. Hakuna ushirikiano wowote kama wanandoa wa kuweza kukaa chini na kushirikishana malengo mbalimbali yatakayoweza kuwasaidia katika kujenga na kuboresha maisha yao.

Sababu kubwa nyingine zilizotolewa kutoka kwenye tafiti kadhaa wa kadha kuwa ndio chanzo cha ndoa nyingi kuvunika na ndoa nyingi ziwe katika foleni ya kuvunjwa, ni Mmonyoko mkubwa wa maadili na ukatili mkubwa wa kijinsia, hasa kwa watoto ni mkubwa inahitaji Watanzania wajipange, hili kutokomeza hili tatizo katika jamii zetu.

Chanzo kingine ni katika vingi ni wivu uliopindukia mipaka, ugumu wa maisha, kuwa na kipato duni, watu kuathirika kiakili, kulazimisha kuingiliana kinyume na maumbile, baadhi ya wenza kuwa na tabia za kishoga, kukosa uaminifu na wenza kupelekea kuchepuka nje ya ndoa zao.

Na Ugomvi wa wanandoa unapelekea watoto kuteseka kwa kukosa malezi bora na hatimaye watoto hao kujikuta wakifanyiwa ukatili wa kingono kutokana na kutokuwa na malezi mazuri kutoka kwa wazazi wa pande zote mbili.

Kuna haja sasa ya serikali kufanya utafiti kupitia wizara zake hili kutengeneza mtaala maalum wa mafunzo ya Jando na Unyago na Mizungu ya kimaisha kwa vijana wa shule za Msingi na Sekondari.

Misamiati

· Kuhuisha, (Huisha): Anzisha tena jambo ambalo lililokuwa limesita kuendelea.

· Jando na Unyago: Mafunzo ya nadhria na vitendo yanayohusu malezi kwa wavulana/wasichana kuhusu mila na desturi za jamii zao

· Mizungu: Matendo ya maarifa ya nyanja mbalimbali ya kimaisha na ya busara ndani ya kumbi yanayofunzwa watu kwa siri.

· Kumbi: Mahali panapofanyika shughuli za jando/unyago

0 comments:

Post a Comment

Je Una Nasaha zozote Kuhusiana na Makala hii?

RAMADHAN KARIM

Read

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!